Jinsi ya kujilinda dhidi ya ujumbe wenye shaka na ulaghai

Kipaumbele chetu kikuu ni kuunda mazingira salama kwa watumiaji wetu kuwasiliana. Tunafanya jitihada za mara kwa mara ili kupunguza barua taka au ujumbe usiotakikana kwenye FaceCall. Ni muhimu kutambua kwamba kama vile SMS za kawaida au simu, watumiaji wengine wa FaceCall ambao wana nambari yako ya simu wanaweza kuwasiliana nawe, iwe wamehifadhiwa kwenye anwani zako au la.

Watumiaji hawa wanaweza kuwasiliana nawe kwa nia ya kukuhadaa ili ufichue taarifa za kibinafsi au za kifedha, au kueneza taarifa zisizo sahihi. Ulaghai umeenea na unaweza kumlenga mtu yeyote, kwa hivyo ni muhimu kuwa na uwezo wa kujitambua na kujilinda dhidi yao.

Nini cha kuangalia katika ujumbe unaotiliwa shaka:

  • Makosa ya uchapaji au sarufi
  • Maombi ya kugonga kiungo, kuwezesha kipengele kipya kupitia kiungo, au kupakua programu
  • Maombi ya taarifa za kibinafsi kama vile kadi ya mkopo au nambari za akaunti ya benki, tarehe ya kuzaliwa, au manenosiri
  • Maombi ya kusambaza ujumbe
  • Maombi ya pesa, au madai yanayodai kuwa unapaswa kulipa ili kutumia FaceCall
  • Kuiga mtu unayemjua
  • Ujumbe unaohusiana na bahati nasibu, kamari, ofa za kazi, fursa za uwekezaji, au mikopo
  • Watu wanaojaribu kupata uaminifu wako kabla ya kuomba taarifa za kibinafsi

Unapopokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye hayuko kwenye anwani zako, tutatoa ishara kwenye ujumbe ili kukusaidia kubaini jinsi ya kujibu. Ishara hizi zitakujulisha ikiwa mtumaji ni mtu unayemjua, ikiwa mna vikundi vinavyofanana, na ikiwa nambari yake ya simu imesajiliwa katika nchi tofauti. Kisha unaweza kufanya uamuzi sahihi kuhusu kama utajibu, kuwaongeza kama anwani, kuwazuia au kuwaripoti.

More Resources

  • Support Team

    Reach our to our Support team for more help! Email us at support@facecall.com

  • Our Support Team is available:

    24/7/365

  • Follow us on Facebook!

    Get the latest news and updates first